Habari za leo ndugu,
Nisiku nyingine tena ambayo Mungu
ametuwezesha kuiona, ni vema kumshukuru Mungu kwa hilo maana ni wengi walitamiani
kuiona siku ya leo lakini hawakuweza.
Ni wakaribishe kwa siku ya leo kushirikiane kujifunza kanuni hizi Tano (5) za mafanikio kiuchumi
ambazo naamini tukizifanyia kazi zinaweza kutusaidia katika kutimiza ndoto zetu;
1.
Jifunze kuweka akiba ya kipato chako:
v Ni
kweli kwamba kipato chetu kinapoongezeka hata mahitaji pia huwa yanaongezeka; lakini
ni vema tukajitaidi kulingana na kipato hicho hicho kidogo angalau tubaki na akiba.
Ni vizuri sana kujiwekea akiba lakini pia ni vizuri zaidi kuweka
akiba yenye malengo, tofauti ha hapo utajikuta unaitumia akiba hiyo kwa vitu
visivyo na manufaa.
Tunaposema akiba wengi huwa tunachanganya tukiamini kuwa
akiba ni kile kinachobakia baada ya matumizi yote, “hapanaa” Akiba ni kile
kiasi kinachotengwa kabla ya matumizi. Kwa mfano umeingiza kiasi 50,000 hakikisha unatemga hata 20% kwa ajili ya kujiwekea akiba
kulingana na kiasi ulichopata kwa siku au mwezi huo.
Kwa kufanya hivyo naamini matokeo utayaona.
2.
Usiwe mtu wa madeni (Kuendekeza madeni).
v
Kwanini
nakwambia “Usiwe mtu wa Madeni”; deni ni Ugonjwa unaoweza kukutoa uhai wako wakati
wowote na saa yoyote. Tumeshuhudia wengi wakijiua/Mali zao kuuzwa kwa sababu ya
kuwa na madeni mengi.
Hata siku moja hutaweze kuwa na maendeleo kama ni mtu wa
madeni, utakuwa mtu wa kuhamisha madeni na itakufanya kuwa mtuwa.
Usinielewe tofauti, sijasema usikope namaanisha usiyaendekeze
yakawa sehemu ya Maisha yako. Kopa kwa malengo na pia ukiwa na uhakika wa
kulipa deni hilo.
Ø
N.B.
Usikope zaidi ya nusu ya kipato chako au mshahara wako maana hutaweza kuulipa
utakufanya uwe mtumwa.
3.
Iheshimu na kuithamini pesa iliyoko mikononi mwako leo.
v
Katika
jamii zetu tumekua na watu ambao ni matajiri sana na wenye uwezo lakini siri
yao kubwa ni kutoidharau pesa, wapo wengi wanakwambia “siwezi kuokota 200/=
hee!” mi mwenzako nikiiona naichukua maana naamini 200/= hiyo inaweza
kunisaidia kupata huduma nitakayoihitaji hata kama ni ndogo.
v
Pesa
unapoitumia vibaya siku zote utaiona ikipita mikononi mwako na hautaifanyia
kitu chochote cha maana. tukiangalia matajiri wengi wanaotuzunguka hawayumbi
kiuchumi kwa sababu wanaijua pesa lakini hawana mazoea na pesa.
v
Hata
kama mfukoni au kenye account yako ya benk una mabilioni ya pesa, jitaidi
uwezavyo kuiheshimu na kuithamini mia moja iliyoko mkononi mwako.
Ø
N.B.
Ebu tujifunze zaidi kuijua pesa na si
kuizoea pesa na kuidharau.
4.
Kuwa na marafiki wanaokupa changamoto au wenye ndoto za kufanikiwa.
v
Nimejifunza
sana katika hili, Ule usemi unaosema “niambie rafiki yako nikwambie tabia yako”;
Huu usemi kila siku unanipa changamoto sana kwamba ile jamii na mazingira
yanayo kuzunguka yanaweza kuwa mchango mkubwa kwa wewe kutokufikia ndoto zako
au mafanikio unayoyahitaji, kwa mfano niambie kuhusu yule mtu ambaye mazingira
yanayomzunguka wengi ni walevi wa kupindukia, wavuta bangi, au marafiki walio
ulio nao vipi wanandoto za kufika mbali? au ni wale ambao wameshaandaliwa kila kitu
na wazazi wao? Vipi maongezi yenu huwa yanahusu nini zaidi? Kuna unachojifunza chochote kulingana na
maongezi yenu ya kila siku?
v
Uhusiano
mzuri na wale watu wanaotuzunguka pia utatufanya tuweze kufikia mafanikio
kupitia frusa tutakazozipata ndani ya jamii zetu; hivyo basi nivema tukaangalia marafiki tulionao na
mchango wao katika mafanikio na katika kusaidiana ili kutimiza ndoto zetu.
5.
Kuwa mtu wa kujifunza kila wakati.
v
Wakati
tunapambana na kutaka kutimiza ndoto zetu za kufanikiwa kiuchumi, tunatakiwa
kuwa watu wa kujifunza; kama ni mwajiriwa tumia muda ulionao kupata ujuzi wa
ziada kulingana na kazi uliyo nayo, kama ni mfanya biashara ongeza juhudi
kuijua zaidi biashara, jifunze zaidi kuyajua mambo yako binafsi. Kama ni kazini
kwako ebu angalia ni kitu gani kimepungua na endapo utakijua zaidi kinaweza
kukuongezea manufaa kazika kazi zako.
v
Mwingine
atapenda kujua ni jinsi gani ataongeza ujuzi?; dunia ya sasa iko mikononi
naamini kwa kutumia simu au computer yako
kwa kuingia mtandaoni hutatoka kama ulivyoingia, soma habari za maana achana na
habari za udaku ambazo zitakupotezea muda wako.
v Tumia muda wako kwa kusoma vitabu, kuhudhuria
tamasha au semina za biashara, ujasiriamali naamini kwa kufanya hivyo utaweza
kuzitimiza ndoto zako za kufanikiwa kiuchumi.
Kwa kumalizia nipende kutoa tahadhari
kwako wewe na mimi ambao tunazo ndoto za kufanikiwa, katika hii safari
tunakutana na changamoto nyingi sana, wapo watakao kukatisha tamaa kuwa
hutaweza, utatengwa na jamii hata ndugu pia kwa kukataa kile wanachokiamini wao
na kukishikilia kile unachokiamini. Naamini kwa kila tunachokifanya
tukimutanguliza Mwenyezi Mungu tutafanikiwa.
Kwa leo niishie hapa, nikuombe wewe
rafiki, ndugu na jamaa ambae umeamua kupambana ili kuifikia ndoto ya mafanikio
uendelee kufuatilia ukurasa huu ili tuendelea kufundishana na kusaidiana kadri
Mwenyezi Mungu atakavyozidi kutubariki.
No comments:
Post a Comment