TABIA 7 ZINAZOWEZA KUKUFANYA KUWA NA UHUSIANO WENYE FURAHA NA WAKUDUMU. - MAARIFA

Breaking

Karibu katika blog ya mariffa kuweza kutambua Ujasiliamali na kujikwamua kiuchumi ahsante

test banner

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Friday, 9 June 2017

TABIA 7 ZINAZOWEZA KUKUFANYA KUWA NA UHUSIANO WENYE FURAHA NA WAKUDUMU.

Image result for love images




Ndugu,Swala la mahusiano limekua ni tatizo sana katika jamii zetu, limekua ni chanzo cha migongano ndani ya jamii, watu kuuana, wengine kujiua, na hata kupelekea walio kwenye ndoa zao kuzikimbia  na kusababisha ongezeko la watoto mitaani wasio na walezi.
Zifuatazo ni Tabia zitakazoweza kuongeza furaha na kufanya mahusiano yenu au ndoa yenu idumu;
  • Kula chakula pamoja;
Image result for love eat together
Inaleta mvuto pale familia inapokaa pamoja kwa ajili ya kupata chakula hasa chakula cha jioni, watu wengi huwa wanaona jambo hili kuwa halina maana yoyote, leo naomba nikwambie ndugu yangu, kuna nguvu kubwa ya upendo na furaha pale munapokaa pamoja na kupata chakula kama familia.
  • Kwenda kulala kwa pamoja

Image result for love sleep
Hii haina maana ya kwenda kufanya ngono kila usiku, bali kwenda kulala kwa wakati mmoja.
Wanandoa  wanakumbushwa kwamba " wanatakiwa kupinga jaribu la kwenda kulala kwa nyakati tofauti" hata kama mtu anabaki  nyuma isiwe kwa muda mrefu.
Pale wanandoa wanapoenda kulala kwa pamoja kwa muda waliojiwekea, inaongeza furaha na amani.
  • Daima kuaminiana na kujaribu kusamehe
Image result for love forgives
Ni wazi hii inategemea na kiwango cha kutokubaliana, lakini nivema mahusiano yenu yakawa ya uaminifu, mwamini mwenzako. Pia tambua hakuna binadamu aliyekamilia, amini kuwa mwenzako amekosea kwa kutokujua na siyo kwa makusudi, mahusiano yenu yaruhusu msamaha na si vinginevyo.
  •  Sema "Nakupenda" na "kuwa na siku njema"
Image result for LOVE
kila asubuhi mwambie mwenza wako au mpenzi wako kumtakia majukumu mema. itamfanya ajisikie vizuri na kuendelea kuiona thamani yako na kuona kuwa unamjali na kumthamini.
  •  Kutumia muda pamoja.
Image result for love SPEND TIME TOGETHER
Tafuteni  muda wa kuwa  pamoja na mwenza wako bila watoto, hii itawafanya kukumbuka  mwanzo wa maisha ya mahusiano yenu kabla ya kuwa na watoto na kufanya upendo wenu uongezeke na kutathimini wapi mumetokea hadi kufikia wakati huo.
wakati mwingine munapaswa kufanya shughuli ya pamoja, si tu kuangalia televisheni.
  • Usisahau kukumbatiaana
Image result for love hUG
Dk Goulston anatuhimiza kukumbatiana na  wapenzi wetu kila siku  (kama hali inaruhusu). "Ngozi yetu ina kumbukumbu ya 'kugusa nzuri',
unapomsalimia mwenzako kwa kumkumbatia kuna mfanya ajisikie kupendwa na kuthaminiwa zaidi.
  • Kushikana mikono;
Image result for love hands together
Wakati mwingine munatakiwa kushikana mikono mukiwa munatembea pamoja. Ni ishara ya umma ya upendo,
Dr. Goulston anashauri kwamba kushikana mikono na mwenza wako  ni ishara ya faraja ya kweli.
  • Mtakie usiku mwema mwenza wako kila usiku.
Image result for love good night
Bila kujali jinsi unavyohisi. Kwa mujibu wa Dk Goulston anasema, hata ishara ya kusema usiku mwema "inamwelezea mpenzi wako kwamba, bila kujali  hali uliyonayo au matatizo yaliyopo au migongano inayojitokeza.
Nimalizie kwa kukushukuru kwa kukubali kutumia muda wako kujifunza na kutaka kujua zaidi juu ya mahusino.

Karibu tuendele kujifunza pamoja.
 
 
 
 

    

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here